Skip to main content

CHEGE CHIGUNDA AUZUNISHWA SANA NA MSIBA WA YP KUTOKA TMK...soma alichokisema hapa..



Saidi Juma maarufu kama  Chege Chigunda Mtoto wa Mama Saidi kutoka TMK ameumizwa sana na Msiba wa mwenzake Yessaya Ambilikile Y.P na Kuyasema haya...

"Innalilahi wa inna ilaih rajiun,sikuwahi kufikiria itatokea siku usiwe karibu yangu nilipigania sana uwepo wako katika kundi letu,wewe ndio ilikua remot yangu ktk uimbaji machozi yananitoka kila dakika nakumbuka mengi naujua msaada wako kwangu,tulipendwa sana kwa sauti zetu kufanana my brother,mungu ndio anajua kwanini ulipojitoa kundini nilipigania mpk uongozi

ukakurudisha,umeniacha ktk Hali ngumu sana na kuiacha Tmk wanaume family ktk majonzi makubwa yasio weza kufutika kirahisi hatuna la kufanya tena kwa sasa tunachofanya nikubaki tunakuombea kwa mwenyezi mungu akupunguzie adhabu na kukuweka mahala pema peponi RIP YP”



Msanii 'YP' toka kundi la TMK Wanaume Family ambaye alfariki jana usiku katika hospitali ya TEMEKE ambako alikuwa akisumbiliwa na kifua kwa muda mrefu lakini hali ilikuwa mbaya katika wiki mbili kabla ya kifo chake.

Meneja wa TMK Wanaume Family Said Fela amethibitisha kutokea kwa msiba huo. Msiba wa msanii huyo uko Keko nyumbani kwa baba yake.

Said Fella amesema Marehemu ambaye jina lake halisi ni Yessaya Ambikile alifanya vizuri na msanii mwingine Y Dash na nyimbo kama 'Ulipenda Pesa', 'Pumzika', 'Shemsha' na nyimbo nyingi za TMK Wanaume Family kama 'Twende zetu' ya Chege, 'Dar mpaka Moro', 'Kichwa kinauma', 'Tufurahi' na nyimbo nyingi za TMK Wanaume family.

THEGREATMULLEY.BLOGSPOT.COM tunamuombea Mungu kaka yetu YP aiweke roho yake mahali pema.

Comments

Popular posts from this blog

EXCLUSIVE AUDIO| CHIKUZEE-KUNGURU MWEUSI|LISTEN AND DOWNLOAD HERE

Baada ya kimya cha muda msanii na mkali wa vocals kutoka hapa Kenya CHIKUZEE ameachia mzigo mpya kutoka NUMBER RECORDS unajulikana kama KUNGURU MWEUSI. Ujio huu wa Chikuzee umekaa tofauti kabisa na alivyozoeleka na mitindo yake ya hapo awali,round hii ameamua kuingia katika mtindo wa TAARAB na ili kuonesha ujuzi wake na mashairi yake yalivyokomaa. Pata kuudownload KUNGURU MWEUSI hapa.. BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD KUNGURU MWEUSI.  

NEW SONG ALERT: NYOTA NDOGO-SUBIRA YANGU| IPAKUE HAPA...

Hii ni ngoma mpya ya msanii wakike NYOTA NDOGO inayokwenda kwajina SUBIRA YANGU ambapo ngoma hii aliweza kuiachia hapo jana. Pata kuipakua hapa ivi upate ujumbe mtamu na Wakuelimisha.

NEW AUDIO | RABBIT KING KAKA FEAT RICH MAVOKO-NJOO | LISTEN AND DOWNLOAD HERE..

Hii ni nyimbo mpya kutoka KenyaTanzania ambapo ni moja ya Colabo iliyongojewa kwa muda mrefu,colabo hio inakwenda kwa jina la NJOO ambapo ni msanii wa Hip Hop ameshirikisha msanii wa Bongo flava kutoka Tanzania hapa nikiwa namzungumzia KING KAKA akiwa na RICH MAVOKO. Nyimbo hio imeachiliwa rasmi hii leo na wasanii hao wawili. pata kuiskiza na ku download hapa..