Katika mkahawa mmoja hapo jana THE GREAT MULLEY ilikuwa na msanii anayetoka katika kundi la X-MATHARE linalotamba na ngoma yao NIMERYKE.
Tuliweza kumuuliza msanii huyo kuwa anaonaje kuhusu usanii wa hapa Kenya,alikiri kuwa hapa Kenya na ulimwengu mzima alidai kuwa hakuna mziki mbaya kabisa ni pesa yako ndio inaongea, "Usanii siku hizi umekuwa sio kipaji tena bali ni pesa yako ndio itakayo kufanya ujulikane na ngoma yako iweze kunye katika anga za ulimwengu" alisema Ohzy.
Tulimuuliza ni ngoma gani anayoonelea sio nzuri lakini ni mfuko ulifanya kazi msanii huyo alicheka na kudai kuwa hataki kusema na kueka wazi maana yeye mwenyewe hataki gumzo na story nyingi mitandaoni lakini aliweza kutupatia mfano wa nyimbo iliyofanya vizuri na kusema kuwa MARY MELA ni ngoma ambayo ililazimishwa katika masikio ya watu lakini hakuwa inaridhisha sana.
Comments
Post a Comment