WANAWAKE WAPINGA KUVULIWA NGUO OVYO OVYO NA WANAUME NCHINI KENYA....soma hapa na utizame picha za maandamano hayo.
Wanawake hapa nchini Kenya mapema hii leo wameandamana
kupinga kitendo cha mwanamke mmoja kuvuliwa nguo wiki jana kwa madai kuwa
alikuwa amevalia sketi fupi sana.
Wanawake
wengi walikerwa na kitendo hicho wakisema kuwa kila mwanamke ana haki ya
kuvalia mavazi yanayomfurahisha.
Hiyo
wiki jana kanda ya video ilisambazwa kwa mitandao ya kijamii ikionyesha
mwanamke huyo ambaye hakutajwa jina hadi sasa akivuliwa nguo zake na wanaume
katika kituo cha magari ya abiria kati kati mwa jiji la Nairobi.
Wanawake mashuhuri
wakiwemo wasanii, wanasiasa na wanaharakati walilaani kitendo hicho wakihoji
kwani mavazi ya mwanamke yanamhusu nini mwanamume ambaye sio mumewe wala jamaa
yake.
Baadhi
walikitaja kitendo hicho kuwa cha kinyama na kinachokiuka haki za wanawake.
Msanii
mmoja mashuhuri Nyota Ndogo alinukuliwa akisema ikiwa wanaume wanawavua nguo
wanawake kwa kile wanachosema ni mavazi yasiyo ya kiheshima, basi na wanaume
wanaolegeza long'i zao na wao basi pia wavuliwe nguzo zao.
Hizi ndizo baadhi ya picha za wanawake hao wakifanya maandamano...
Comments
Post a Comment