Kundi la wanamgambo nchini Somalia Al Shabaab limekiri
kuwaua watu 36 katika shambulio lililotokea kwenye machimbo ya kokoto karibu na
mji wa Mandera kaskazini mwa Kenya.
Katika taarifa iliyotolewa kwenye mtandao wa kundi hilo, wanamgambo hao
wamesisitiza kuwa ndio waliowaua wakenya hao kwa sababu ya majeshi ya Kenya
kuendelea kuwa nchini Somalia. Taarifa za mauaji hayo zilitolewa kwa mara ya kwanza na Shirika la Msalaba Mwekundu.
Wakazi wa eneo hilo wamesema waathirika wote wa tukio hilo ni watu wasio Waislam ambao walikuwa wakifanya kazi katika machimbo hayo yaliyopo Kormey kilomita 15 kutoka mji wa Mandera Kaskazini mwa Kenya.
Tukio hili linafuatia tukio la wiki moja iliyopita ambapo watu wapatao 28 waliuawa katika shambulio la basi la abiria huko Mandera.
Kundi la wapiganaji wa Kiislam la Al
Shabab limekiri kuhusika na mauaji hayo.
Mkuu wa Polisi hilo amesema bado
wanafuatilia tukio hilo.
Katika tukio lingine, mtu mmoja
ameripotiwa kuuawa nchini kufuatia mlipuko katika klabu moja ya usiku katika
mji wa Wajir kaskazini mwa Kenya.
Basi walimokuwa wakisafiria wakenya
wengine waliouawa na Al Shabaab mjini Mandera wiki iliyopita
Kwa mujibu wa Kamishna wa Polisi wa
Wajir, Frederick Sishia, shambulio hilo limefanyika saa mbili usiku na kuua mtu
mmoja na watu wengine wanne wamejeruhiwa.
Washambuliaji hao walitumia
magruneti na silaha nyingine za kijeshi kufanya shambulio hilo.
Wiki iliyopita watu wengi waliuawa
eneo la Mandera kaskazini mwa Kenya.
Kenya imejikuta ikilengwa na mashambulio
ya kigaidi tangu majeshi yake yapelekwe nchini Somalia kukabiliana na
wapiganaji wa Al Shabab. Mbali na miji ya kaskazini mwa Kenya kushambuliwa kila
mara, miji mikubwa nchini humu ya Nairobi na Mombasa imekuwa ikilengwa na
mashambulio ya kigaidi.
Source:BBC SWAHILI
Comments
Post a Comment