Msanii Mez B aka Moses aliyekuwa Mkoani Dodoma kwa matibabu baada ya kurudishwa nyumbani na mama yake amefariki Dunia.Inasemekana kuwa msanii Mez B alikuwa akisumbuliwa na homa ya mapafu [TB] na alikuwa kwenye dozi na leo ilikuwa siku ya tatu toka anatumia dawa hizo.
Leo asubuhi kulingana na mtandao wa Sammisago.com aliamka na kunywa dawa na chakula ila hali yake haikuwa sawa na kuonekana amelegea. Daktari wake alipigiwa simu na kuamuru awekewe drip ila hali yake ikawa mbaya zaidi, wakati wanampeleka hospitalini alifia walipofika mapokezi. Jirana amelezea haya.
Kumbuka msanii Mez B aliimba nyimbo kama KASUKU WANGE,NIMEKUBALI na KAMA VIPI aliyomshirikisha msanii wakike Ray-C a.k.a Rehema Chalamila.
Pole kwa familia ya Mez B, Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema, Amen.
Comments
Post a Comment