Msanii kutoka hapa Kenya anayetambulika kama hit maker wa HIDAYA na NGOMA ITAMBAE ambapo zote ameshirikisha msanii Chikuzee hivi karibuni atakuwa anaachia ngoma yake mpya inayojulikana kama IHALE.
Msanii Susumila wakati huu inaonekana hatomshirikisha CHIKUZEE katika ngoma hio mpya kama watu walivyo tarajia kuwa ngoma nyengine pia watakuwepo pamoja.
Kumbuka ngoma hizo mbili waliposhirikiana fununu zilizuka kuwa wawili hao wanataka wawe kama kundi moja na kupiga nyimbo zao wakiwa pamoja,Tukimuhoji msanii SUSUMILA alituelezea kuwa yeye na Chikuzee sio kundi moja bali walikuwa wakiimba t kama wasanii wengine tulimnukuu " Mimi na Chiku hatuko kundi moja na wala hatuna mkataba tulikuwa na fanya kazi tu na sio ati Chiku na Susu ni kundi kama wat wanavyo sema lakini kukitokea kazi kama inahitajika tuifanye mimi na yeye ttapiga kazi" alisema Susumila
Susumila atakuwa anaachilia ngoma yake mpya itakayojulikana kama IHALE ambpo amemshirikisha msanii kutoka Congo anayetambulika kama SARKOZY.
Kaa mkao wa Kula.
Comments
Post a Comment