Skip to main content

BENSO AFUNGUKA KUHUSIANA NA VIDEO YAKE YA "IMEREMENDE"....Soma hapa..



Msanii kutoka Mombasa/Kenya Benso ambaye pia aliweza kushinda tuzo ya mwana muziki bora wa kiume katika tuzo za mwaka jana katika COAST MUSIC AWARDS hii leo amefunguka kuhusiana na video yake alioachia mapema wiki hii.


Tuliweza kukutana na BENSO na tukaweza kumuulia maswali kadhaa kuhusiana na karia yake ya mziki msanii huyo aliweza kusema kuwa yeye katika jambo hujiamini ndio maana hufanya kazi zake kiuwakika bila kuangalia na amefanya nini ama nini kinachoendelea katika mziki.

Tuliweza kumuuliza video aliyoitoa imemgharimu pesa ngapi ama kiwango gani cha pesa haya ndio aliyasema " Kiukweli siwezi sema video ni pesa ngapi lakini kiukweli imenigharimu na me hupenda ni gharamike ili mafans wangu na familia yangu ya mashabiki wawezekuona kazi nzuri na ni navyo jituma kimziki" Alisema.


Benso aliweza pia kufunguka kuwa video hio yake mpya kwa jina IMEREMENDE kuna sehemu aliitajika kuingia ndani ya BOMAS OF KENYA alioko jijini Nairobi ivo aliweza kuenda nakuifanyia video na hio na pia sehemu nyengine aliweza kulipa watu sehemu ya County ya Kilifi ili aweza kuchukua video hio tulimuuliza kuwa watu hao ama wakaaji hao aliweza kuwalipa pesa ngapi pia alisema kuwa hio ni siri yake na wakaazi hao wa Kilifi.


Kumbuka pia msanii Benso mbali na mziki ni mwanabiashara na anaumiliki wa kampuni kadhaa katika katikati ya jiji la Mombasa na kusema mbali na mziki yeye hufanya biashara zake lakini mziki ndio ameupa kipao mbele maana anajiamini anaweza na pia ana talanta ya uimbaji na mtindo wa kurap.

Tazama Video mpya hapa hio hapa..

Comments

Popular posts from this blog

EXCLUSIVE AUDIO| CHIKUZEE-KUNGURU MWEUSI|LISTEN AND DOWNLOAD HERE

Baada ya kimya cha muda msanii na mkali wa vocals kutoka hapa Kenya CHIKUZEE ameachia mzigo mpya kutoka NUMBER RECORDS unajulikana kama KUNGURU MWEUSI. Ujio huu wa Chikuzee umekaa tofauti kabisa na alivyozoeleka na mitindo yake ya hapo awali,round hii ameamua kuingia katika mtindo wa TAARAB na ili kuonesha ujuzi wake na mashairi yake yalivyokomaa. Pata kuudownload KUNGURU MWEUSI hapa.. BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD KUNGURU MWEUSI.  

NEW SONG ALERT: NYOTA NDOGO-SUBIRA YANGU| IPAKUE HAPA...

Hii ni ngoma mpya ya msanii wakike NYOTA NDOGO inayokwenda kwajina SUBIRA YANGU ambapo ngoma hii aliweza kuiachia hapo jana. Pata kuipakua hapa ivi upate ujumbe mtamu na Wakuelimisha.

NEW AUDIO | RABBIT KING KAKA FEAT RICH MAVOKO-NJOO | LISTEN AND DOWNLOAD HERE..

Hii ni nyimbo mpya kutoka KenyaTanzania ambapo ni moja ya Colabo iliyongojewa kwa muda mrefu,colabo hio inakwenda kwa jina la NJOO ambapo ni msanii wa Hip Hop ameshirikisha msanii wa Bongo flava kutoka Tanzania hapa nikiwa namzungumzia KING KAKA akiwa na RICH MAVOKO. Nyimbo hio imeachiliwa rasmi hii leo na wasanii hao wawili. pata kuiskiza na ku download hapa..