Mziki ni safari ya milima na mabonde tambarare na pakavu ikiwa umeona msanii amefika juu na kuwa staa kama DIAMOND PLATNUMZ,JOSE CHAMELEON,WYRE na wengine wengi basi jua wameyapitia na walioyapitia ni vile hujapata kuskiza ama kujua stori zao walipotokea hadi hapa walipofika kuna wengine wametaka hata kuachana na mambo ya mziki kwasababu ya walioyapitia laki9ni jamii ndio hufwapa motisha na kuendelea.
Leo hii tumepatana na msanii ANTHONY JACKSON kwa jina la usanii ni ZIKY WA ZIKY kutoka mkoani pwani msanii huyu ni moja wa wasanii wanao kuja vizuri na wenye sauti nzuri pamoja na idea zenye kufunza.
Ni msanii mwenye umri wa miaka 23 ambaye anamilikiwa na studio za JUNGLE MASTERS chini ya produza EMMY DEE pamoja na uongozi wa JOS K MADALA,ni moja wa kijana anayepata maisha magumu kimziki na kimaisha anaishi maeneo Pwani Kusini (SOUTH COAST) na ni msanii ambaye elimu yake iliishia katika darasa la nane (CLASS 8) na hana mzazi ata mmoja ana umiliki wa mdogo wake alioachiwa na wazazi wake ambapo huyo mdogo wake ndio anamtegemea msanii huyo kwa kila hali na sasa wameweza kuungana na kufungua biashara lakini msanii ZIKY bado anahangaikia kazi za mijengo
kupitia mahojiano yake ya moja kwa moja na PILIPILIFM katika kipindi cha MWAKE MWAKE kinachoongozwa na DOUBLE C(CHRISS na CHIGULU) msanii Ziky aliweza kusema kuwa alishawahi kufukuzwa na aunty yao katika nyumba walio kuwa wanaishi kwasababu hawakuwa na kazi ya kufanya na mara yakwanza aliposkia mziki wake katika kituo cha radio aliweza kutoa machozi ya furaha na hakuweza kula.
Skiliza live interview hio hapa chini....
Comments
Post a Comment