CHAPA-TIZZOH KUWABANIA VIJANA WANAO KUJA KWA KASI ZAIDI WANAOJULIKANA KAMA WASIOJALI BAND..Soma hapa zaidi..
Mapema wiki hii kumekua na vuta nikute kutoka kwa management ya vijana wanaokuja kwa kasi sana wanaojulikana kama WASIOJALI BAND na msaniimkongwe kutoka Mombasa anayetambulika kama CHAPA-TIZZOH.
Kuna ngoma moja ambayo inagombaniwa na wasanii hao ambao ni Tizzoh pamoja na kundi la vijana wannne wanaojulikana kama WASIOJALIBAND, katika ngoma hio kuna sauti ya mkali wa HIDAYA ambaye ni SUSUMILA inasemekana ngoma hioiliweza kurekodiwa mwaka huu mapema ambapo wasanii wawili ndio walio weka sautiambae ni TIZZOH pamoja na SUSUMILA na ngoma kutungwajina la JIRANI.
Kulingana na management ya WASIOJALIBAND inasemekana waliweza kuiskia nyimbo hio na msimamizi wa vijana hao kuipenda nyimbo hio na kutaka kugharamikia video yake lakini pasi na sauti ya Tizzoh,nyimbo hio iliweza kurekodiwa tena lakini sauti ya Tizzoh iliweza kuondolewa na wale vijana kuchukua mistari hio hio na kuijaza sauti na nyimbo ilipokamilika ikapachikwa jina lile lile la JIRANI na ikawa ni nyimbo ya WASIOJALIBAND wakiwa na SUSUMILA.
Ally Babaz ambaye ndie meneja wa wasanii hao aliweza kuisikiliza nyimbo hio tena na kuipata iko sawa kilichokua kimebakia ni ngoma hio kuachiliwa na maandalizi ya video yaanze bila kupoteza muda lakini mambo yalibadilika pale CHAPA-TIZZOH alipopata taarifa yakwamba nyimbo imeguezwa na iko karibu kuachiliwa,Tizzoh alikimbia studio na kukutana produza NOIZER ambapo alimwambia kuwa nyimbo hio isiweze kuachiliwana lau ikiachiwa na yeye pia ataweza kuachia ile ya kwake alikuwa amefanya na SUSUMILA.
Hivi sasa hizo nyimbo mbili ziko hewani zinapigana matsumbi ikiwemo ya CHAPA-TIZZOH akiwa na SUSUMILA na WASIOJALIBAND wakiwa na SUSUMILA swali ni je ni sauti ya Susumila ndioinayopiganiwa ama ni nini kinachopiganiwa katika nyimbo hio JIRANI?
Nyimbo hzio zote mbili utaweza kuzi download hapa hapa katika THEGREATMULLEY.
Comments
Post a Comment