EXCLUSIVE STORY| UNAKIJUA KILICHO SABABISHA RABIZZLE NA SIS P KUACHANA NA KUMKIMBILIA PRODUZA KHALID WA AMILLION RECORDS?.Pata story nzima hapa
Hii leo ndani ya kipindi cha MASHAV MASHAV UNIVERSITY kinachoongozwa na GATES MGENGE msanii wakike SIS P alikua kikaangoni ambapo aliweza kutiririka majibu bila kusita.
GATES MGENGE.
Gates Mgenge aliweza kumuuliza msanii huyo wakike kwamba uhusiano wake na Rabizzle uko vipi naye aliweza kusema kwamba ameachana na Rabizzle kwasababu ambazo asingeweza kuzitamka lakini alijikuta ghafla anatamka kwamba RABIZZLE alikua akimtelekeza kwamba alikua akimpiga saa zote kwa kosa dogo tu "Rabizzle tuweza kuachana kitambo na sababu zilinifanya tuachane sio zaidi ya moja maana kuna wakati pia alinipiga karibu nipelekwe hosipitali jambo ambalo liliweza kuni kwaza sana."
Rabizzle
Gates aliweza kumuuliza kama Produza Khali ni mchumba wake ama ni msanii tu kama wasanii wengine Sis P aliweza kusitasita lakini mwisho kusema kwa Khalid ndie mume wake mtarajiwa na pia sio sio kwa vile ni mtu wake wa karibu basi atakua anafanya kazi AMILLION aliweza kusema kwamba produza KHALID alimpa ruhusa ya kufanya kazi katika studio yoyote hapa nchini.
Sis P aliweza kusema kwasasa yuko chini ya AMILLION RECORDS na sio chini ya RABBIZZLE kama ilivyokuwa mwanzo.
Msanii huyo ameweza kuachilia ujio wake mpya unaokwenda kwa jina BONGE LA BWANA ambapo video yake iko njiani na muda wowote inatarajiwa kuachiliwa video hio inaemekana imgharimu nusu Milioni.
Comments
Post a Comment