NEW VIDEO ALERT| EDDY TICHA ADAI KWAMBA AMECHOKA KUSKIKA SAUTI,TAZAMA "ZAWADI" VIDEO YAKE MPYA
Baada ya kuwaporomoshea mashabiki zake nyimbo album mzima bila video hapo mwaka jana msanii aliyetimia vocals na uandishi EDDY TICHA amejitokeza katika kioo chako.
Wimbo huu unakwenda kwa jina ZAWADI ambapo video imeweza kuandaliwa na LYNKE JR kutoka kampuni ya DA MUSIK LAB na audio yake kuketiwa chini na produza Morbiz (Sheriff) ndani ya studio za THURNDER SOUND.
Baada ya kimya cha muda msanii na mkali wa vocals kutoka hapa Kenya CHIKUZEE ameachia mzigo mpya kutoka NUMBER RECORDS unajulikana kama KUNGURU MWEUSI. Ujio huu wa Chikuzee umekaa tofauti kabisa na alivyozoeleka na mitindo yake ya hapo awali,round hii ameamua kuingia katika mtindo wa TAARAB na ili kuonesha ujuzi wake na mashairi yake yalivyokomaa. Pata kuudownload KUNGURU MWEUSI hapa.. BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD KUNGURU MWEUSI.
Hii ni ngoma mpya ya msanii wakike NYOTA NDOGO inayokwenda kwajina SUBIRA YANGU ambapo ngoma hii aliweza kuiachia hapo jana. Pata kuipakua hapa ivi upate ujumbe mtamu na Wakuelimisha.
Hii ni nyimbo mpya kutoka KenyaTanzania ambapo ni moja ya Colabo iliyongojewa kwa muda mrefu,colabo hio inakwenda kwa jina la NJOO ambapo ni msanii wa Hip Hop ameshirikisha msanii wa Bongo flava kutoka Tanzania hapa nikiwa namzungumzia KING KAKA akiwa na RICH MAVOKO. Nyimbo hio imeachiliwa rasmi hii leo na wasanii hao wawili. pata kuiskiza na ku download hapa..
Comments
Post a Comment