Skip to main content

EXCLUSIVE STORY||| NYOTA NDOGO AWATOA POVU WANAOTETA MBONA HAZEEKI

Staa wa kike wa muziki wa kizazi kipya hapa nchini Kenya maarufu kama Nyota Ndogo, amewajibu watu wanaoonekana kumfuatilia maisha yake binafsi.

Nyota ambaye alizaliwa mwaka 1981, amekuwa kwa game ya muziki tangia mwaka wa 2004 ambapo tokea hapo amekuwa akitoa hits za muziki kila anapoingia studioni kurekodi.

Muziki kwake umekuwa kila kitu, na si mara moja amekuwa akihoji kwenye vituo vya habari kuwa hata nyumba anayoishi kwa sasa imejengwa na pesa za muziki pamoja na biashara nyingine ambazo zinazidi kumtilia kipato cha kila siku.

Nyota ni baadhi ya mastaa wa muziki wa nchini Kenya wanaoheshimika sana, na pia amekuwa katika mstari wa mbele katika wale mastaa wakongwe nchini Kenya ambao hawakosi show kila wakati.

Hata hivyo mbali na mafanikio hayo, Nyota Ndogo katika maisha yake ya kawaida hakosi kupitia changamoto za kimaisha kama staa wengine Afrika. Leo kupitia ukurasa wake wa Facebook, Nyota ametupia ujumbe unaonekana kuwasuta watu fulani wenye kupenda kumdadisi maisha yake binafsi hadi kufikia kiwango cha kumuuliza kwanini yeye hazeeki.

Naye mwanadada huyu, hajasita kuwajibu wanaouliza maswali kama haya kwa kuuandika ujumbe ulioambatana na picha yenye kumuonyesha akiwa na tabasamu kubwa kwenye kipaji chake cha uso…nikinukuu, Nyota ameandika: Wanasema why uzeeki nyota nawajibu nakubali matokeo and I smile all the time, sijui kukasirika kwa mda mrefu ila ikifikia hapo basi umeniumiza sana.”

Comments

Popular posts from this blog

EXCLUSIVE AUDIO| CHIKUZEE-KUNGURU MWEUSI|LISTEN AND DOWNLOAD HERE

Baada ya kimya cha muda msanii na mkali wa vocals kutoka hapa Kenya CHIKUZEE ameachia mzigo mpya kutoka NUMBER RECORDS unajulikana kama KUNGURU MWEUSI. Ujio huu wa Chikuzee umekaa tofauti kabisa na alivyozoeleka na mitindo yake ya hapo awali,round hii ameamua kuingia katika mtindo wa TAARAB na ili kuonesha ujuzi wake na mashairi yake yalivyokomaa. Pata kuudownload KUNGURU MWEUSI hapa.. BONYEZA HAPA KU-DOWNLOAD KUNGURU MWEUSI.  

NEW SONG ALERT: NYOTA NDOGO-SUBIRA YANGU| IPAKUE HAPA...

Hii ni ngoma mpya ya msanii wakike NYOTA NDOGO inayokwenda kwajina SUBIRA YANGU ambapo ngoma hii aliweza kuiachia hapo jana. Pata kuipakua hapa ivi upate ujumbe mtamu na Wakuelimisha.

NEW AUDIO | RABBIT KING KAKA FEAT RICH MAVOKO-NJOO | LISTEN AND DOWNLOAD HERE..

Hii ni nyimbo mpya kutoka KenyaTanzania ambapo ni moja ya Colabo iliyongojewa kwa muda mrefu,colabo hio inakwenda kwa jina la NJOO ambapo ni msanii wa Hip Hop ameshirikisha msanii wa Bongo flava kutoka Tanzania hapa nikiwa namzungumzia KING KAKA akiwa na RICH MAVOKO. Nyimbo hio imeachiliwa rasmi hii leo na wasanii hao wawili. pata kuiskiza na ku download hapa..